June 18, 2013




Kipa Iker Casillas amecheza mechi yake ya 800 akiwa mchezaji wa kulipwa.

Rekodi hiyo angweza kuifikia miezi miwili au mitatu iliyopita lakini ilishindikana kwa kuwa kocha wa zamani wa Real Madrid, Jose Mourinho aliamua kumuweka nje kwa kuwa walikuwa na tofauti zao.

Casillas ametimiza rekodi hiyo ya mechi 800 wakati akiichezea timu yake ya taifa katika mechi ya Kombe la Mabara dhidi ya Japan.


Katika michuano hiyo inayoendelea nchini Brazil, pamoja na kukaa muda mrefu nje ya uwanja, Casillas alisema alijiona kama ndiyo anaanza kucheza soka la kulipwa.

“Nilijiona kama ndiyo mpya, mambo yalikwenda tofauti kabisa. Lakini nashukuru kila kitu kimekwenda vizuri na furaha yangu inaonekana wazi,” alisema.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic