June 13, 2013





Kocha Patrick Liewig tayari ametua jijini Dar es Salaam kuendelea na kazi ya kuinoa.

Liewig amesema amekuja kuendelea na kazi yake kwa kuwa yeye ndiye kocha mkuu wa Simba.

“Mimi ndiyo kocha, nitaanza kazi leo au kesho. Nimejua wanafanya mazoezi Kinesi. Nitakwenda kuanza kazi,” alisema.

Alisema anashangazwa na kuona viongozi wa Simba wanaonyesha kumkwepa, lakini hajali.


“Niko hotelini hapa Kariakoo, inaitwa Supphire. Hivyo nitaendelea kuwa hapa huku nikiwatafuta viongozi,” alisema.

Tayari Simba imeishangia mkataba wa miaka miwili na Abdallah Kibadeni kuinoa Simba.

Mkataba wake unaonyesha, Simba wanalazimika kumlipa mshahara wa miezi miwili ambao ni dola 12,000.

Simba ilimuondoa Milovan Cirkovic kwa mtindo huo, lakini alirejea kutoka kwao Serbia na kudai mshahara wake hadi alivyolipwa na Malkia wa Nyuki dola 35,000.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic