June 13, 2013



 
Wakati Yanga imetangaza kujitoa katika michuano ya Kagame Cup, mabingwa wa Kenya, Tusker nao wametangaza kujiondoa.

Kwa mujibu wa mtandao wa SuperSport wa Afrika Kusini, Tusker pia imejitoa kutokana na kutokuwa na uhakika kuhusiana na usalama kwa kuwa moja ya miji itakayofanyika michuano hiyo ni Darfur.

Mmoja wa maofisa wa Tusker, Charles Obiny ameiambia SuperSport kwamba wameamua kujitoa kutokana na kutokuwa na uhakika wa usalama nchini Sudan.


“Haukuwa uamuzi lahisi, lakini baada ya mjadala wa kutosha, tumeamua kujitoa mara moja kwa kuwa hata waandaaji (Cecafa) wameonekana kushindwa kuthibitisha usalama. Hivyo tunafanya hivyo kwa wachezaji wetu,” alisema Charles Obiny.

Tusker imekuwa timu ya pili kujitoa baada ya Yanga ya Tanzania huku Simba na Falcon za Zanzibar nazo zikielezwa

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic