June 27, 2013




Iingawa imepita, lakini kati ya vivutio vilivyojitokeza katika mechi kati ya Taifa Stars dhidi ya Ivory Coast baada ya kipa namba moja wa timu hiyo Boubacar Barry kumpa mtoto mmoja aliyekuwa uwanjani pale glovu zake.

Kipa huyo anayekipiga katika timu ya Lokeren ya Ubeligiji alitoka kama kawaida kwenda kupasha misuli na wachezaji wenzake.
 
JAMAA ANATAKA KUCHUKUA GLOVUZ KWA DOGO..
Baada ya takribani dakika 20 za kufanya mazoezi ya kutosha Boubakar maarufu kama Copa alianza safari ya kurejea vyumbani na wenzake.

Akiwa amefika nyuma ya benchi la Ivory Coast alimuona mtoto huyo anayekadiriwa kuwa na miaka nane hadi kumi, mara moja alielekea upande wake na kumrushia glovu zake mbili.

WANANCHI WANAMKOMALIA JAMAA..
Dogo ambaye jina lake halikujulikana mara moja naye alikuwa ‘shap’, aliinuka na kuzidaka glovu hizo lakini ajabu mtu mwingine anayekadiriwa kuwa na miaka 25 hadi 30 aliinuka na kutaka kuzichukua kwa madai yeye ndiye alimuita kipa huyo hadi akazirusha.
 
DOGO MSHINDI WA MCHEZO..
Lakini juhudi zake zilikwama baada ya watu waliokuwa eneo hilo kutaka amuachie bwana mdogo huyo glovu zake hizo zilizokuwa na jina la Copa.
Jamaa hakuwa na ujanja, pamoja na kulaumu dogo huyo alibaki na glovu hizo na mwisho akaziinua kuashiria ushindi na watu wakamshangilia kwa nguvu.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic