June 27, 2013



Jamaa mwenyewe ni huyo mwenye traksuti nyeusi, angalia mkononi anavyochana hiyo karatasi huku akiendelea kusoma maneno, pia kama daktari, angalia alipokaa..
Mechi kati ya Ivory Coast dhidi ya Taifa Stars ilikuwa na vituko vingi, si lahisi vikawa simulizi ya siku moja kwa kuwa ilikuwa na upinzani mkubwa na kikosi cha wageni kiliundwa na nyota wengi katika soka duniani.

Ivory Coast pamoja na kuwa ugenini ilifanikiwa kuibuka na ushindi wa mabao 4-2 na kufuta matumaini ya Watanzania kucheza Kombe la Dunia kwa mara ya kwanza.
 
Hawa ndiyo madaktari wa kweli...angalia hata sehemu walipo na vifaa vyao..
Pamoja na uwezo waliounyesha Ivory Coast, kitu cha ajabu kabisa ni mmoja wa memba wa benchi lao la ufundi kuonekana akifanya kazi zilizoonekana wazi kuwa ni za kishirikina.




Kwa nini mshirikina?
1.     Kwanza mtu huyo ambaye mwanzo alitambulishwa kama daktari wa timu, hakuwa akifanya kazi hizo na wengine ndiyo walikuwa ‘bize’. Lakini ukifuatilia, utagundua hakuwa amekaa sehemu ambayo anaweza kukaa daktari kama ambavyo madaktari wa kweli walipokuwa wamekaa.

2.     Alionekana muda mwingi akifuatilia mchezo kuliko hata wachezaji wenyewe huku akiwa ameshika karatasi mkononi halafu akawa anazungumza kama mtu anayesali.


3.     Baadaye aliendelea kusema maneno lakini safari hii zile karatasi alizokuwa nazo mkononi alikuwa akizichana moja baada ya nyingine.

4.     Kuonyesha alikuwa ni mtu wa kubandikwa kwenye benchi, hakuwa hata na siti. Hivyo alilazimika kuibia siti za wachezaji na waliporudi, alipiga makoti nyuma ya viti vya wachezaji na kuendelea na kazi yake.

5.     Baada ya mechi, wakiwa vyumbani, wakati madaktari wa timu wakiendelea kuwa ‘bize’ na wachezaji, yeye alikuwa busy akifunga vitu vyake huku akiandika mambo kadhaa na baada ya hapo akakaa pembeni kimyaa.

1 COMMENTS:

  1. unahushahidi au mastor ya town???? andika vitu vyenye mantiki

    ReplyDelete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic