June 26, 2013




Kamati ya Utendaji ya klabu ya Simba inakutana kesho jioni kujadili masuala mbalimbali na kubwa ni kuhusiana na usajili wao.

Katika suala la usajili, kamati hiyo ya utendaji itajadili na kupata jibu sahihi kuhusiana na kipa Juma Kaseja kwamba kama iendelee kubaki naye au la.


Chanzo cha ndani kutoka ndani ya Simba kimeeleza Kaseja hakupata nafasi ya kufanya mazungumzo na uongozi wa Simba baada ya kutaka kukutana na Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili, Zacharia Hanspope na si mtu mwingine.

“Ukweli kuhusiana na suala la Kaseja ni kwamba bado hatujakuwa na jibu la uhakika na lazima kamati ya utendaji ikutane na kupata jibu la mwisho kuhusiana na hilo.

“Hivyo kesho jioni tutakuwa na jibu na tumeelezwa Kaseja yuko kwao Kigoma ana masuala ya kifamilia. Lakini sisi tutakaa na kujua.


“Awali alikuwa azungumze na Mzee Kinesi lakini yeye akasisitiza lazima azungumze na Hans Pope yeye mwenyewe. Tunaendelea kusubiri kuhusiana na hilo halafu tutajua baadaye ni vipi.

“Mwanzo pia kulikuwa na mazungumzo na Kaseja lakini akasema dau kubwa, hivyo naweza kusema bado hakuna jibu sahihi kuhusiana na kubaki au kuachwa na ukiangalia muda wa usajili bado kabisa, unaweza kusema sasa ndiyo usajili umefunguliwa,” kilieleza chanzo cha uhakika.

Mara kadhaa kumekuwa na taarifa kwenye vyombo vya habari kwamba Simba imeachana na Kaseja na anatua Azam FC, lakini mara zote viongozi wa Simba wamekuwa akitaka kuwepo kwa sbira.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic