June 7, 2013



Kocha wa Chelsea, Jose Mourinho amempa onyo nahodha wa timu hiyo, John Terry kuwa anaweza kumuweka benchi kama ambavyo alivyofanya kocha wa muda aliyepita klabuni hapo, Rafa Benitez kama hata onyesha uwezo mzuri.

Mourinho ambaye ametua Chelsea hivi katibuni akitokea Real Madrid, amesema kuwa atapanga wachezaji kwa kufuata faida yao kikosini na siyo kuangalia jina la mtu.

Akiwa Real Madrid, kocha huyo alimweka benchi bila huruma nahodha wa timu hiyo, Iker Casillas licha ya kuwa alikuwa kwenye kiwango kizuri.

“Mimi ndiyo kocha, nitampanga mchezaji kutokana na kiwango chake, mchezaji anapata nafasi anapoonyesha uwezo mazoezini.

“Ilikuwa kawaida kwangu kumuacha (Marco) Materazzi, ndivyo ninavyoweza kufanya kama alivyofanya Benitez mwaka huu kwa Terry,” alisema Mourinho.




0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic