June 28, 2013



Kiemba akiwa na Ngassa wakati akiwa Simba...
Kiungo wa Simba, Amri Kemba amepishana na mamilioni kutoka kwenye moja ya klabu za nchini Ureno, lakini amepata nafasi nyingine ya kufanya kazi na Waisrael.

Simba walipata ofa kutoka Ureno juu ya mchezaji huyo lakini ikaweka dili hilo pembeni kwa kuwa walikuwa kwenye mazungumzo na Klabu ya Raja Casablanca ya Morocco, ambayo pia ilikuwa ikimhitaji mchezaji huyo.


Zakaria Hans Pope ambaye ni Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya Simba ameliambia Championi Ijumaa kuwa klabu yake imepokea ofa kutoka kwa klabu moja kubwa ya nchini Israel inayomuhitaji Kiemba.

Alisema klabu hiyo ambayo hakutaka kuitaja jina lake inamhitaji Kiemba na wametoa ofa kwa dola 200,000 (Sh milioni 320), ingawa Simba imesema bei ya mchezaji huyo ni dola 400,000 (Sh milioni 640).

“Waisraeli wanaonyesha nia ya kumuhitaji sana kutokana na kila mara wamekuwa wakitutumia barua pepe wakitaka tuwajibu juu ya hatua tuliyofikia.

“Tunahitaji fedha lakini hatutaki kufanya mambo kihuni, tunasubiri kwanza Raja Casablanca tuwasikie wamefikia wapi ila kwa hao Waisrael wakishuka kwenye dau kidogo kama dola 300,00 au 250,000 tutakubali,” alisema Hans Pope.
SOURCE: CHAMPIONI

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic