June 6, 2013

Pele akiwa na Neymar na Messi..
Gwiji la soka duniani, Pele amesema alikuwa kati ya watu waliomzuia Neymar kwenda kucheza soka nchini England.

Pele amesema anaamini kwa Neymar kwenda Hispania ni wazo zuri kuliko England.

Katika mahojiano na redio moja nchini Brazil, Pele alisema alimuambia Neymar asiende England baada ya kumueleza kuna timu zinamuhitaji.
„Ingekuwa tatizo kwake kutoka Brazil na kwenda kucheza katika ligi wanayotumia nguvu nyingi. Ingemsumbua, hivyo nikamshauri asiende,“ alisema Pele.

Neymar amejiunga na Barcelona na tayari imeishakuwa gumzo kuhusiana na atakavyoshirikiana na mkali wa timu hiyo, Lionel Messi.

Lakini yeye Neymar amesema atamsaidia Messi kuendelea kuwa mchezaji bora wa dunia, kitu ambacho wengi wanaona haitakuwa sahihi.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic