June 13, 2013





Mshambuliaji Wayne Rooney wa Man United, ametinga katika shoo ya mwanadada Rihanna akiwa amenyoa katika staili mpya.

Katika shoo hiyo iliyofanyika kwenye Uwanja wa Old Trafford jijini Manchester, Rooney alitinga ukumbini hapo akiwa na mkewe Coleen na kusababisha awe kivutio kikubwa.



Pamoja na shoo hiyo, lakini siku hiyio ilikuwa muhimu zaidi kwa  Rooney na mkewe Coleen ambao walikuwa wakitimiza miaka mitano ya ndoa yao.
Miaka kadhaa iliyopita, Rooney alilazimika kutumia mamilioni ya fedha kufuta kipara lakini safari hii alionekana akiwa ampunguza nywele zote na kuonekana kama upara tena.



Rooney anahusishwa na kuondoka Man United na timu ambazo tayari zimeonyesha nia ya kutaka kumsajili ni Chelsea, Arsenal na Paris St Germain ya Ufaransa.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic