July 1, 2013



BUYINZA (KUSHOTO) WAKATI AKIKIPIGA KCCA KABLA YA KUTUA VIETNAM..

Simba imeonyesha imepania kurekebisha makosa yaliyoisumbua msimu uliopita baada ya kumchukua beki mwingine Mganda kutoka Vietnam kuja kujiunga na timu hiyo.

Beki huyo, Asuman Buyinza anatarajia kutua nchini kesho na kuanza mazoezi na Simba chini ya Kocha Abdallah Kibadeni.


Habari za uhakika kutoka ndani ya Simba zimeeleza Buyinza atakuwa katika kikosi cha Simba kwa wiki mbili akifanya mazoezi na Kibadeni ndiye atatoa uamuzi.
Miaka miwili iliyopita, Buyinza alikuwa beki tegemeo na nahodha wa KCCA ya Uganda kabla ya kujiunga na klabu kubwa ya Vietnam ya Da Nanga kwa dau la dola 50,000.


“Kweli anakuja nchini na tayari ameishatumiwa tiketi. Tumeelezwa ni beki mzuri na tumemfuatilia kwa muda,” kilieleza chanzo.

“Lakini mfumo wa ufanyaji kazi wa Simba kwa kipindi hiki ni kuliacha benchi la ufundi lifanye kazi yake, hivyo tutamuachia kocha aamue baada ya kuiona kazi yake,” kilieleza chanzo cha uhakika.

Simba ina beki mwingine Mganda, Samuel Ssenkoomi ambaye anatokea URA ya nchini humo ingawa kutokuwa na kimo kirefu imekuwa sababu inayowapa hofu mashabiki wa Simba.

Hata hivyo, Ssenkoomi ameonyesha kujiamini kwamba anaijua kazi yake, lakini bado hajaonyesha cheche zake baada ya kukumbana na mkasa wa kuumia, siku chache baada ya kutua nchini.

Msimu uliopita, Simba ilisumbuka sana katika safu hiyo ya ulinzi na hasa beki wa kati hasa baada ya kuondoka kwa Kelvin Yondani na kujiunga na Yanga.

Mchezaji mwingine ambaye pia ni Mganda ambaye Simba inahaha kumpata ni Moses Oloya ambaye pia anakipiga katika timu ya Xuan Thahn Sai Gon ya Vietman pia ingawa Yanga nayo imeanza kutia mkono ikionyesha kuwa na ‘njaa; pia ya kumpata Oloya ingawa mambo yamekuwa yakifanyika kwa siri kubwa.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic