SEHEMU YA PILI NA YA MWISHO....
Na Saleh Ally
Ukisia jina la Mohammed Bin Slum, moja
kwa moja utaelekeza mawazo yako katika mambo mawili, soka na biashara ya
matairi ya magari.
Bin Slum ni mfanyabiashara maarufu zaidi
katika biashara ya matairi na betri za magari. Lakini ndiye mdhamini mkuu wa
klabu ya Coastal Union ya Tanga.
Pamoja na kuwa mdhamini, Bin Slum ni
Mkurugenzi wa Ufundi wa Coastal Union maarufu kama Wagosi wa Kaya.
Mwendo wa timu hiyo kwa misimu miwili
pamoja na usajili wa msimu ujao, unaifanya Coastal Union kurudisha heshima na
umaarufu wake wa miaka ya 1980 na kuingia kwenye mbio za moja ya timu
zinazoweza kuwa bingwa
.
Katika mahojiano maalum na Championi
Jumatatu, Bin Slum ambaye alizaliwa na kukulia mkoani Tanga kabla ya kuhamia
jijini Dar es Salaam mwaka 1994 baada ya kumaliza kidato cha sita, anazungumzia
masuala kadhaa kuhusiana naye lakini pia Coastal Union.
Bin Slum ambaye amewahi kuwa mchezaji wa
timu ya NBC Tanga na timu ya mkoa huo ya Tanga Stars ambayo ilikuwa inaundwa na
wachezaji wengi kutoka Coastal Union na African Sports ‘Wana Kimanumanu’,
anaamini Coastal itafanya vizuri zaidi msimu huu.
Salehjembe: Mmewachukua Boban na
Nyosso, Simba wamewaondoa kwa sababu ya
nidhamu…
Bin Slum: Nawajua vizuri sana Boban na Nyosso, ni watu
ambao tunaishi karibu na tunashirikiana katika mambo mengi ya mpira. Sitaki
tufanye kitu kwa kuamini wengine, huenda kuna viongozi au kiongozi wa Simba
alikuwa na matatizo nao binafsi, kayaingiza hadi kazini.
Salehjembe: Hivyo mmeamua kujaribu kama
moto unaunguza?
Bin Slum: (kicheko), hatuna maana hiyo.
Huenda Simba hawakuwapa second chance (nafasi nyingine) ili waone kama
watajirekebisha. Utaona tumewapa mkataba wa mwaka mmoja kila mmoja. Hapo tuna
nafasi ya kuangalia na kuhakikisha ingawa mimi ninaamini watacheza.
Salehjembe: Coastal Union inaonekana ni
kati ya Big Four za Ligi Kuu Bara? Vipi hauna hofu ya kuingia kwenye football
fitna na hujuma?
Bin Slum: Najua una maanisha kuonewa
labda kwa kuwa tunatokea mikoani, mimi siamini kama TFF au kuna mtu anaweza
kufanya hivyo.
Huenda Simba na Yanga zinaweza kuvuta kutokana na maslahi,
lakini tunajiamini na tutakachofanya ni maandalizi ya kutosha.
Salehjembe: Labda wapi mnapanga kufanya
maandalizi, mtaweka kambi Tanga au nje ya Tanzania?
Bin Slum: Ninaamini tutakwenda nje ya
Tanzania. Ni suala tunalolifanyia kazi, kama kila kitu kikikamilika, basi tutao
taarifa.
Salehjembe: Simba ndugu yao Coastal
Union, wewe pia ni shabiki wa Simba?
Bin Slum: Nimelipenda hili swali, unajua
kasumba iliyopo ni kila Mtanzania lazima awe Yanga au Simba, si kweli. Mimi si
shabiki wa timu yoyote kati ya hizo mbili, tokea nimezaliwa ni Coastal Union.
Salehjembe: Inaonekana ni vigumu kwa
Watanzania wengi, wewe umeweza vipi?
Bin Slum: Baba yangu alinishika mkono
tokea nikiwa mdogo kwetu Tanga kwenda uwanjani kuiona Coastal Union. Zamani
mikoani, watu walikuwa mashabiki wa timu zao na Yanga au Simba, ndiyo maana
zilipata tabu zilipoenda mikoani maana watu walishangilia timu zao. Nafikiri
hata sasa ifikie iwe hivyo.
Salehjembe: Mara ngapi umeona mechi za
Simba na Yanga zilizokuvutia?
Bin Slum: Hata mara moja, sijawahi
kwenda uwanjani kuziona Yanga na Simba zikipambana, imewahi kutokea hivyo mara
mbili na niliona mechi kwenye runinga. Sioni sababu ya kwenda uwanjani kwa kuwa
hizo si timu zangu, bora niende nikaione Coastal inacheza mechi ya kirafiki.
Salehjembe: Maana yake zikicheza Yanga au
Simba hata na timu nyingine hauendi uwanjani?
Bin Slum: Hapana, nimewahi kuziona
zikicheza lakini mara nyingi kama zinacheza na timu nyingine, mfano Yanga na
JKT Ruvu au zinapokuja kucheza na Coastal Union.
Salehjembe: Nini kinakuvutia zaidi kwa
Yanga na Simba na unaamini mkijifunza au kukipata basi mtapiga hatua?
Bin Slum: Sidhani kama wana kitu kizuri
kama idadi kubwa ya mashabiki, natamani ingekuwa ni ya Coastan Union. Kwetu
ingekuwa biashara kubwa, angalia wao hata biashara ya jezi tu hawafanyi kwa
kuwa hawana jezi inayotambulika ni ya Yanga au Simba. Coastal Union tuna jezi
inatambulika kokote, wao hawana na wamewaachia wajanja wachache wanajiingizia
mamilioni. Ndiyo maana unaweza kusema Simba na Yanga wana rangi tu.
Salehjembe: Kwa miaka yote uliyoishi
nini Dar es Salaam, vipi Yanga au Simba hawajawahi kukuomba kusaidia?
Bin Slum: Kweli wamenifuata mara nyingi
sana kujaribu kunishawishi niingie na kusaidia klabu hizo. Lakini nimekataa,
mimi ni Coastal Union na ninahitaji kuisaidia ili irejee katika hadhi yake.
Najua wao ni timu kubwa, lakini tutapambana.
SOURCE: CHAMPIONI
SOURCE: CHAMPIONI
0 COMMENTS:
Post a Comment