July 19, 2013



Beki wa Simba, Shomari Kapombe anaondoka nchini leo kwenda Uholanzi kwa ajili ya kufanya majaribio ya kucheza soka la kulipwa.

Kapombe anaondoka ikiwa ni baada ya TFF kuridhia maombi yake ya kuondoka katika kikosi cha timu ya taifa na kwenda kufanya majaribio. 

Awali shirikisho hilo lilimzuia na kuharibu ratiba yake ya majaribio hali iliyofanya wakala wake, Denis Kadito kulalama.


Msemaji wa Simba, Ezekiel Kamwaga amethibitisha kuwa Kapombe atafanya majribio kwa siku hizo 14 akiwa nchini humo.

Suala la timu anayofanya majaribio bado halijawekwa wazi, ingawa Mwenyekiti wa Simba, Ismail Aden Rage alisema atajaribiwa FC Twente lakini wakala wake amekuwa akisisitiza suala hilo ni siri na hajawahi kutaja ni timu gani atafanya majaribio zaidi ya nchi.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic