July 19, 2013


KIGGI (KUSHOTO) AKIMDHIBITI NGASSA WAKATI WAKIWA SIMBA PAMOJA..


Kiungo kinda wa Simba, Kiggi Makasi ameamua kwenda kwa waganga wa kienyeji kwa ajili ya kulitibu goti lake.

Rafiki wa karibu wa Kiggi, amesema kinda huyo ameamua kufanya hivyo na mganga anayeaminika anaweza kumtibu yuko mjii Bagamoyo.

“Kweli Kiggi ameamua kwenda kwa mganga kwa kuwa amepania kurudi uwanjani, lakini mimi naona kama si kitu kizuri.

“Nimejaribu kumshauri lakini imeshindikana kwa kuwa hata akibaki hawezi kupata matibabu na viongozi wa Simba wamekuwa wagumu kupokea simu zake,” alisema rafiki huyo.

Alipoulizwa Kiggi kuhusiana na suala la kwenda kwa mganga, hakutana kuzungumzia zaidi lakini akasema analazimika kuhaika ili kupona na kurejea uwanjani.


“Lazima nihangaike ndugu yangu, nataka kurudi uwanjani lakini masuala ya mganga tuachane nayo, kikubwa ninachotaka kurejea ni uwanjani,” alisema.

Tayari Mwenyekiti wa Simba, Ismail Aden Rage alisema mchezaji huyo atapatiwa matibabu kama ambavyo daktari bingwa aliyeshauri apelekwe nchini India kwa ajili ya matibabu. Lakini hadi sasa imekuwa kimya.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic