July 19, 2013



Beki Mbuyi Twite ataikosa mechi ya keshokutwa wakati Yanga itakapowavaa URA, timu inayomilikiwa na kampuni ya watoza kodi ya mapato ya Uganda.

URA itakuwa nchini kucheza mechi mbili za kirafiki, ikianza na Simba kesho kabla ya kuivaa Yanga, keshokutwa kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.

Twite amesema ataikosa mechi hiyo kutokana na kusumbuliwa na maumivu ya goti ingawa amekuwa akifanya mazoezi taratibu.


“Kwa sasa niko kwenye usimamizi wa daktari wa timu, naendelea kupata matibabu hivyo nimeona vizuri kama nitakaa nje ili nipone vizuri,” alisema.

Awali Yanga ilikuwa icheze mechi ya kirafiki dhidi ya 3 Pillars ya Nigeria, jana lakini ikagundulika timmu hiyo ilikuwa bagumashi kupita kiasi.

TFF ikapoga stop mchezo huo kwa kuwa Wanigeria hao walikuwa wameokotana lakini walitaka kucheza na mabingwa wa Tanzania.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic