July 6, 2013


NGASSA SIKU YA KWANZA MAZOEZINI YANGA..

*Azungumzia tena kuhusu Msuva, asisitiza namba Yanga hazina mwenyewe
 Na Saleh Ally
KOCHA Mkuu wa Yanga, Ernie Brandts anaanza msimu mpya ambao utakuwa na mambo mengi sana lakini kikubwa zaidi ni kuthibitisha kama kweli alichokifanya msimu uliopita hakikuwa ni cha kubahatisha.

Brandts ameanza maandalizi ya msimu mpya baada ya Yanga kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu Bara. Huu ndiyo msimu mgumu zaidi kwa kocha huyo Mholanzi ambaye anataka kikosi chake kuwa na maandalizi mazuri zaidi.

Pamoja na usajili, Brandts ambaye anasema wazi kuwa bado anamhitaji mshambuliaji Moses Oloya Mganda anayekipiga nchini Vietnam lakini ujio wa Mrisho Ngassa nao umekuwa ni gumzo kubwa sana.
 
BRANDTS AKIWA MAZOEZINI SIKU YA KWANZA MSIMU HUU..
Anasema anajua kwamba Ngassa ni gumzo kutokana na umaarufu wake na uwezo alionao na amekuwa akifanya vizuri katika soka ya Tanzania kwa kipindi kirefu sasa.

Lakini anasisitiza kwamba katika kikosi chake kila mchezaji yuko sawa na mwingine, hakuna mwenye uhakika na namba zaidi ya kumuonyesha kocha anastahili kucheza. Maana yake, Ngassa atatakiwa kufanya mambo matatu makubwa ili kuendelea kupata nafasi katika kikosi chake.


Ngassa alianza mazoezi juzi, kwa mara ya kwanza kocha huyo akamuona Ngassa akifanya mazoezi chini yake na siku iliyofuata akampa ruhusa ajiunge na kikosi cha timu ya taifa, Taifa Stars kinachojiandaa na michuano ya Kombe la Chan. Stars itacheza na Uganda ikianzia nyumbani.

SALEHJEMBE: Nini hasa Ngassa anatakiwa kufanya ili kuwa mchezaji wa kikosi cha kwanza?
Brandts: Kunaweza kuwa na mambo mengi sana, lakini matatu yatakuwa muhimu sana kwangu. Kwanza kabisa ni kuhusu kujituma, lazima afanye hivyo kwa kuwa ana kipaji. Lakini bila ya kujituma, hakuwezi kuwa na tofauti na mwenye kipaji na asiyenacho.

SALEHJEMBE: Pili na tatu ni kipi?
Brandts: Kucheza kwa faida ya timu, mara kadhaa nimeangalia mechi alizocheza akiwa Simba. Lazima ajue mchezaji anafanya kila analoweza kuisaidia timu yake. Hivyo Ngassa lazima aweke hayo kichwani wakati akiitumikia Yanga.

SALEHJEMBE: Malizia jambo la tatu.
Brandts: Kuna mabadiliko anayotakiwa kuyafanya kiuchezaji, nafikiri nitazungumza naye mwenye na kumueleza. Wakati akicheza Simba au timu ya taifa nimekuwa nikiyaona. Najua ana kipaji cha juu sana, hivyo hayo mambo lazima ayafanyie kazi.

SALEHJEMBE: Labda utakutana naye lini?
Brandts: Sasa ana majukumu ya timu ya taifa na tayari nimetoa ruhusa kwa wachezaji walio na kikosi cha Taifa Stars, lakini atakaporejea mazoezini, basi nitazungumza naye na huu ni utaratibu wa kawaida wa kuzungumza na wachezaji wote ikiwezekana kila mmoja kwa wakati wake.

SALEHJEMBE: katika siku yake ya kwanza ya mazoezi na Yanga, kuna kitu umeona?
Brandts: kitu kipi?

SALEHJEMBE:  Ambacho anacho Ngassa na huenda kimekuvutia?
Brandts: Amenifurahisha kwanza kuwahi, pili alifanya mazoezi kwa kujituma na huenda akaendana na ninachokitaka. Ingawa kuna kitu kidogo alikosea na nikamuonya.

SALEHJEMBE:  Siku ya kwanza tu, kitu gani?


SALEHJEMBE: Unafikiri kuwa na mchezaji nyota kama Ngassa kunaweza kukusumbua?
Brandts: (Tabasamu) Mimi nilikuwa mmoja wa nyota wa Uholanzi ambao walicheza Kombe la Dunia. Huenda ni nyota zaidi, lakini nidhamu yangu iko juu na ndiyo maana kazi yangu inafanikiwa. Nimesisitiza sana la kujituma, hili linajumuisha nidhamu ambayo ni sehemu ya mafanikio.

SALEHJEMBE: Ngassa ni winga, awali ulikuwa ukimtumia Simon Msuva, ndiyo kusema sasa ataozea benchi?
Brandts: Kila mchezaji ana nafasi yake Yanga, hapa muhimu ni suala la kujituma kutoka kila upande. Kama nilivyosema, Yanga hakuna mchezaji mwenye uhakika wa namba asilimia mia. Kila mmoja lazima ajitume kuoyesha anataka na anaweza kuisaidia timu.

SALEHJEMBE:  Bado haujajibu kuhusu Ngassa na Msuva?
Brandts: Ndiyo nimejibu, labda nifafanue zaidi. Kutokana na juhudi zao mazoezini, Msuva na Ngassa wote wanaweza kucheza kutokana na viwango vyao vilivyo au anaweza kucheza Msuva halafu Ngassa akakaa nje, inategemea anajituma vipi mazoezini.

SALEHJEMBE:  Kwani utatumia mfumo upi?
Brandts: Mifumo ni mingi, iko ambayo atacheza mmoja na mwingine kubaki benchi, lakini kuna mfumo ambao wanaweza kucheza wote. Hapa itategemea viwango vyao na wenyewe wako katika viwango vizuri kiasi gani, hasa kutokana na ninachokiona mazoezini.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic