July 14, 2013






Manchester United imetua jijini Sydney nchini Australia kwa ajili ya ziara yake ikiwa inajiandaa na msimu mpya.

Wachezaji kadhaa wa timu hiyo wamekuwa kivutio kikubwa lakini Kocha mpya, David Moyes ameonyesha ni tofauti na yule wa zamani, Alex Ferguson.

Tofauti kwa kuwa alikuwa akifanya mambo kadhaa kama vile kupiga picha sehemu ambazo zinamvutia.




Moyes alipiga picha daraja maarufu la Sydney pamoja na jingo la Opera House ambalo ni moja katika ya majengo maarufu duniani.

Kawaida Ferguson amekuwa hatoi hata simu mfukoni wala kusumbuka kupiga picha, badala yake muda mwingi amekuwa akifanya tofauti kabisa.
Lakini Moyes ameonyesha si mtu wa kujivunga na anaweza kuwa huru kufanya mambo yake.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic