| Brian Majegwa akimtoka Ngassa. |
Kocha Mkuu
wa Uganda, Milutin Sredojevic ‘Micho’ amesema hawezi kuingilia uhuru kiungo
Brian Majwega kuzungumza na timu yoyote, lakini akamuonya.
Majegwa ,20,
ambaye alitoa krosi safi iliyozaa bao lililoiua Taifa Stars katika mechi ya
kuwania kucheza fainali za Chan Afrika Kusini, tayari Yanga na Simba zimeanza
kumfukuzia.
| Micho kazini. |
Lakini Micho
amesema Majegwa anayekipiga KCCA ya Uganda anaweza kuzungumza na timu yoyote
lakini akamtaka kuwa makini na kuangalia jukumu lililo mbele yake la timu ya
taifa.
“Hauwezi
kumzuia mchezaji asizungumze na timu, mimi si kiongozi wa klabu yake. Lakini
naweza kumuasa kama mwalimu wa timu ya taifa.
“Kwamba mbele kuna jukumu zito ambalo lazima alitekeleze, la sivyo atakuwa katika sehemu ambayo si sahihi. Hivyo aangalia kuwa timu ya taifa sasa ina mechi muhimu ya marudiano.
“Kwamba mbele kuna jukumu zito ambalo lazima alitekeleze, la sivyo atakuwa katika sehemu ambayo si sahihi. Hivyo aangalia kuwa timu ya taifa sasa ina mechi muhimu ya marudiano.
“Asichanganye
mambo lakini Yanga au Simba, kama wamevutiwa naye, wanaweza kuzungumza na klabu
yake kwanza kwa maana ya kufuata utaratibu.
Tayari Yanga
ndiyo zaidi imeonyesha kuvutiwa na kiungo huyo ambaye alikuwa kero kwa mabeki
wa Stars.







0 COMMENTS:
Post a Comment