July 14, 2013




Mshambuliaji mpya wa Simba, Hamis Tambwe ameondoka kurejea kwao Burundi ikiwa ni siku moja tu baada ya kusaini mkataba wa miaka miwili Msimbazi.

Tambwe amerejea kwao kumaliza majukumu na atacheza mechi mbili muhimu, moja dhidi ya Sudan kuwania kucheza Chan na ya pili akiwa na timu yake ya Vital’O.

Mshambuliaji huyo amesaini mkataba wa miaka miwili kuichezea Simba, tayari akiwa ni mfungaji bora wa michuano ya Kagame iliyofanyika nchini Suda.

Lakini Tambwe pia ni mfungaji bora wa Ligi Kuu ya Burundi na alifunga mabao 18 yaliyompa nafasi hiyo. Msimu mmoja kabla alikuwa mfungaji bora namba mbili baada ya kufunga mabao 16.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic