July 11, 2013




MAKOCHA WA ZAMANI WA YANGA, MICHO NA TIMBE WAKIWASILI LEO DAR NA KIKOSI CHA THE CRANES TAYARI KUIVAA TAIFA STARS...
   

Kocha Mkuu wa Uganda, Milutin Sredojevic ‘Micho’ ametoa kali leo wakati akitua jijini Dar es Salaam na kikosi chake cha The Cranes.

The Cranes watakuwa wageni wa wanaume, Taifa Stars katika mechi ya kuwania kucheza fainali za Chan itakayopigwa keshokutwa Jumamosi kwenye Uwanja wa Taifa, Dar.

Micho amesema hata kama Taifa Stars itakuwa nyumbani, bado kikosi chake ni bora zaidi na wachezaji waliokuwa wanampa hofu ni Mbwana Samatta na Thomas Ulimwengu tu.


“Kweli Taifa Stars ina kikosi kizuri, lakini hofu yetu kubwa ilikuwa Ulimwengu na Samatta. Lakini sasa tutapambana vilivyo,” alisema Micho.
“Simaanishi dharau kubwa, lakini ninaweza kusema tunataka kushinda hapa. Wala msitegemee tutacheza kwa kujilinda.


“Mimi na msaidizi wangu (Sam Timbe) si wageni na soka la Tanzania. Hivyo tutacheza na tumejiandaa,” alisema.



Kikosi cha The Cranes kimefikia katika Hoteli ya Sapphire iliyoko Kariakoo jijini Dar es Salaam.

Mashabiki kadhaa walijitokeza kwenye Uwanja wa Ndege wa Julius Nyerere (JNIA) kuwapokea wachezaji hao watakaovaana na Stars Jumamosi.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic