July 20, 2013

KIGGI (KULIA) AKIWA NA SIMBA
Klabu ya Simba imeamua kukata mzizi wa fitna na kumpeleka kiungo wake Kiggi Makasi kutibiwa nchini India.

Taarifa za Kiggi kupelekwa India zimepatikana jioni hii jijini Dar es Salaam na kuthibitishwa na Katibu Mkuu wa Simba, Evodius Mtawala.


Mtawala amesema suala hilo si geni lakini tayari uhakika kuwa Kiggi atakwenda India kwa matibabu.

“Tayari tuliishatangaza kuhusiana na kumpeleka India na tulichokuwa tunasubiri tupate nafasi kwa daktari bingwa.

“Sasa ndiyo ametueleza na maandalizi yameanza, hivyo Agosti katika terehe iliyopangwa atakwenda India kwa ajili ya matibabu,” alisema.

Kutokana na kuona Simba wamechelewa kumpeleka India, Kiggi aliamua kwenda kwa mganga wa kienyeji mjini Bagamoyo.

Kiggi aliamua kuutibu mguu wake huo alioumia wakati Simba ikiwa mkoani Dodoma katika mechi ya kirafiki dhidi ya CDA.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic