July 19, 2013




Wenger akiwa na Stojkovic...
Stojkovic wakati akiwa mchezaji wa Grampus...

Kocha Arsene Wenger amerejea katika mji wa Nagoya nchini Japan ambayo aliondoka mwaka 1996 na kujiunga na timu hiyo ya England.

Mfaransa huyo alikuwa kocha wa timu ya Nagoya Grampus, safari hii amerudi na timu yake hiyo ya England ambayo ilimuona akiwa mjini hapa na kumpa kazi.
 
Wenger akipokelewa...

Wenger ametua mjini hapo na kupokelewa kwa heshima kubwa huku akiaminika ndiye kocha kutoka Ulaya kwenye mafanikio makubwa zaidi kuliko wengine waliowahi kuifundisha Nagoya.




Wenger ambaye alipokelewa kwa heshima kubwa alisifia hatua kubwa waliyopiga kisoka.

Lakini kivutio kikubwa zaidi kilikuwa ni kocha wa Nagoya Grampus, Dragan Stojkovic ambaye alisajiliwa na Wenger katika nafasi ya ushambuliaji wakati yeye akiwa kocha.

Walipokutana katika meza wakati wanazungumza na waandishi wa habari, Wengwer alionyesha kuwa ni mwenye furaha kumkuta mwanafunzi wake akiwa ndiye kocha wa timu yake hiyo ya zamani.

Hali hiyo inaonyesha ujuzi wa kocha huyo umeendelea kuwa kumbukumbu kwa mashabiki ambao wanamchukulia kama shujaa.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic