August 15, 2013





Kiungo nyota wa Tottenham, Gareth Bale ameishuhudia timu yake ya taifa ya Wales ikicheza mechi ya kirafiki dhidi ya Jamhuri ya Ireland akiwa kwenye benchi.

Kocha Mkuu wa Wales, Chris Coleman amethibitisha kuwa kweli Bale ni majeruhi ndiyo maana aliamua kumkalisha katika benchi akiwa na suti yake kama mtazamaji.


Mechi hiyo iliyokuwa na upinzani mkali dhidi ya majirani hao ilimalizika kwa sare ya bila kufungana.


Lakini wachambuzi wanaona suala hilo kama kuna ujanja na huenda Bale anafanya hivyo ili kuendeleza kampeni zake za kutaka kujiunga na Real Madrid.


Inaonekana kuwa Bale asingeweza kucheza mechi hiyo kwa kuwa tayari alishaileza Spurs kwamba yeye ni mgonjwa.


Hivyo amekuwa akikwepa kujiunga na Spurs ikiwa ni sehemu ya kampeni ya kuendeleza kupewa ruhusa ili ajiunge na Madrid.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic