August 15, 2013





Mshambuliaji mpya wa Simba, Betram Mombeki yuko katika hatari ya kuongezeka uzito na kupungua kasi nchini kutokana na kula vyakula ambavyo si sahihi kwa wanamichezo.

Mombeki ambaye ameonekana kuwa tegemeo katika upachikaji mabao kwa washambuliaji wa Simba, alionekana katika mgahawa mmoja katika eneo la Mlimani City akila chakula ambacho ni kuku wenye mafuta kwa wingi maarufu kama ‘junk food’.
 
MOMBEKI TAYARI KWA JUNK FOOD KWENYE MHAGAWA HUO....
Akiwa katika mgahawa huo, Mombeki aliyeongozana na kiungo Humud Abdulhalim ambaye hakuka chakula.

Baada ya Mombeki kuchukua chakula hicho  na kuongozana na Humud katika maegesho ya magari ambako walipanda gari aina ya Mazda rangi ya bluu lililokuwa likiendeshwa na Humud.


Kwa mujibu wa madaktari na mitandao maalum ya afya, vyakula hasa kuku wa mafuta wanaouzwa katika migahawa maalum ni hatari sana.

Wachezaji wanaocheza ligi kubwa barani Ulaya wamekuwa wakikatwa na madaktari.

Junk food au kwa jina jingine la fast food huongeza haraka sana mafuta (fat) mwilini ambayo huzunguka vifaa maalum vya mwili kama moyo.

Moyo wenye mafuta ni hatari kwa mwanamichezo yoyote kwa kuwa unakuwa umebanwa wakati unatakiwa kuwa huru.

Lakini kuongezeka uzito si kitu kizuri kwa mchezaji, kwani pamoja na kusababisha kasi yake ipungue, lakini uzito mkubwa unaweza kuchangia kuumia kwa viungo kama magoti na kifundo cha mguu ‘enka’.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic