August 15, 2013





Mshambuliaji mpya wa Yanga, Mrisho Ngassa ambaye anakabiliwa na sakata la uhamisho kutoka Simba, amenunua gari jipya aina ya Toyota Prado.


Gari hilo linalokadiriwa kufikia thamani ya Sh milioni 50, ameanza kulitumia takribani wiki sasa na amekuwa akienda nalo mazoezini.
Prado la Ngassa ni ghali zaidi kuliko magari yote yanayotumiwa na wachezaji na makocha wa timu hiyo.


Kocha Mkuu, Ernie Brandts pia anatumia Prado lakini thamani yake ni chini kidogo ukilinganisha na lile la Ngassa kwa kuwa yanapishana model na mwaka wa kutengenezwa.

Kabla Ngassa alikuwa akimiliki gari aina ya Nissan ambalo alianza kulitumia baada ya kuliuliza lile la Toyota Verrosa alilokuwa amepewa na Simba baada ya kujiunga nayo.

Simba inaeleza ilimpa gari hilo na fedha ili kuongeza mkataba wa mwaka mmoja baada ya kuwa limemchukua kwa mkopo kutoka Azam FC.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic