August 7, 2013


Bango linalomuonyesha kiungo Gareth Bale wa Tottenham kwa ajili ya kutangaza Ligi Kuu England katika jiji la New York limeondolewa haraka.

Bango lililokuwa nje ya ukumbi maarufu wa Times Square limeondolewa ikiwa ni siku moja tu baada ya Bale kuchelewa mazoezini.

Kuchelewa kwake mazoezini kumeelezwa ni sehemu ya vituko anavyofanya akiwa amepania kwenda Real Madrid.


Inaonekana sasa umefikia wakati Bale hatazuiliwa kwenda Madrid na hata televisheni ya NBC iliyokuwa imeweka bango hilo imelitoa ikiamini Bale sasa atakuwa mshiriki wa La Liga na si Premiership.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic