August 14, 2013



Kikosi cha Coastal Union ya jijini Tanga imeondoka leo na kutimkia jijini Mombasa, Kenya kwa ajili ya kwenda kukipiga na timu ya Bandari FC inayoshiriki Ligi Kuu ya nchini humo.

Aidha, pamoja na Coastal kucheza mechi hiyo ya kirafiki na Bandari, pia itacheza mechi nyingine mbili na timu za nchini humo kwa ajili ya maandalizi ya Ligi Kuu Bara inayotarajiwa kuanza Agosti 24, mwaka huu.

Mashambulizi ya kikosi cha Coastal msimu huu yataongozwa na kiungo Haruna Moshi 'Boban' ambaye amejiunga na timu hiyo akitokea Simba.
 
Hemed Morocco ambaye ni Kocha Mkuu wa Coastal, aliliambia Championi Jumatano kuwa, wameamua kuchagua kucheza na timu za Kenya akiamini timu za huko zina ushindani mkubwa, hivyo zitawajenga kisoka.


“Tutacheza mechi tatu za kirafiki tukiwa Mombasa, tayari tumeshafanikisha mipango ya kucheza na Bandari lakini pia tutacheza na nyingine mbili kwa ajili ya kujiweka vizuri zaidi.

“Unajua timu za kule ni nzuri kwa ajili ya ushindani wao mkali mara zote unapokutana nazo, kwa hiyo itatusaidia sana sisi kujijenga na baadhi ya vitu kwenye soka,” alisema Morocco.

Coastal pia itatumia ziara hiyo kwa ajili ya kuweka kambi nchini humo ambapo bado haijawekwa wazi itakuwa ni ya siku ngapi.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic