August 14, 2013



 Mchezaji wa zamani wa timu ya Yanga na timu ya taifa, Taifa Stars, Godfrey Bonny ‘Ndanje’,  ametua timu ya Lipuli FC ya Iringa na kusaini mkataba wa mwaka mmoja wa kuitumikia klabu hiyo.

Bonny amemaliza mkataba wa kuitumikia timu ya Saoswat Youth Club ya nchini Nepal msimu uliopita, hivyo amerudi nchini na kumwaga wino Lipuli inayoshiriki Ligi Daraja la Kwanza.


Akizungumza na Championi Jumatano, katibu mkuu wa klabu hiyo inayonolewa na mchezaji wa zamani wa Yanga, Shadrack Nsajigwa, Willy Chikweo, alithibitisha uwepo wa mchezaji huyo klabuni hapo. 

“Kila kitu kimeshakamilika, tayari tumeshamalizana na Bonny na amesaini mkataba wa mwaka mmoja kwa ajili ya kuitumikia klabu yetu katika msimu ujao wa Ligi Daraja la Kwanza,” alisema Chikweo.

Lipuli kwa sasa ipo katika mikakati mizito ya kuirejesha timu hiyo Ligi Kuu Tanzania Bara tangu iliposhiriki mara ya mwisho kwenye ligi hiyo msimu wa 1998/99.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic