August 6, 2013



Staa wa Barcelona, Lionel Messi alilazimika kuweka majukumu yake ya uwanjani pembeni kwa muda nchini Thailand na kujumuika na watoto wenye ulemavu kwa ajili ya kucheza na kufurahi nao pamoja.


Messi ambaye ni mshindi mara nne wa tuzo ya Ballon d'Or alijumuika na watoto hao ambao wengi wao walionekana kufurahia uwepo wake kwenye kituo chao hicho ambapo, Messi alikuwa pamoja na kipa wa Barcelona, Jose Manuel Pinto ikiwa ni sehemu ya majukumu ya Unicef ambao ndiyo walioandaa utaratibu wa shughuli hiyo.

Wachezaji hao walisaini vitabu na jezi za kumbukumbu za watoto hao kwenye kituo hicho kilichopo jijini Bangkok

Barcelona ipo nchini humo ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya msimu ambapo itakipiga dhidi ya timu ya taifa ya Thailand, kesho Jumatano huku Neymar aliyesajiliwa kwa pauni milioni 50 kutoka Santos, hivi karibuni akiwa ni mmoja ya mastaa watakaocheza mechi hiyo.



0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic