August 12, 2013


AKIAGWA NA OFISA WA FIFA...

 Na Saleh Ally, aliyekuwa Zurich USWISS
 Mtanzania Damas Ndumbaro ametua katika makao makuu ya Shirikisho la Soka la Kimataifa (Fifa), tena kimyakimya.

Championi lililokuwa na mwaliko katika makao makuu ya shirikisho hilo jijini humo, baadaye lilimuona Ndumbaro akiingia kwenye mkutano na baadhi ya maofisa wa shirikisho hilo.

Dakika kadhaa, alitoka na kuingia katika chumba kingine ofisini hapo ambako alikaa kwa takribani dakika 15 na kutoka.
 
..AKIWA NA BAADHI YA MAOFISA WA FIFA WAKIWEMO WAAMUZI NA WAKUFUNZI KUTOKA NCHINI SWEDEN...



Alipoulizwa kilichompeleka Fifa, Ndumbaro ambaye ni wakala wa wachezaji anayetambuliwa na shirikisho hilo, alisisitiza kwamba mambo yote yanabaki kuwa siri yake na maofisa hao.

Kuhusiana na tetesi kwamba ana mpango wa kugombea nafasi ya urais wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) inayoshikiliwa na Leodegar Tenga kwa sasa, Ndumbaro alisema:
 
AKITOKEA KATIKA MOJA YA LIFTI ZA JENGO LA FIFA AMBAKO ALIJICHIMBIA..
“Huu ulikuwa ni mwaliko maalum, kuna mambo mengi ya muhimu kuhusiana na maendeleo ya soka la Tanzania. Sidhani kama ni sahihi kwenda kwenye vyombo vya habari kwa kuwa yanahitaji utekelezaji kwanza.

“Mimi nakushauri usubiri, acha niingie katika utekelezaji halafu baadaye nitazungumza ni nini hasa,” alisema.

Ofisa wa Fifa aliyekuwa anamuaga Ndumbaro na kumkabidhi vitabu vya Fifa, pia aligoma kuliongelea suala hilo na kusisitiza anayeweza kufanya hivyo ni Ndumbaro.

“Mwenyewe anaweza kulizungumzia hilo, mimi kazi yangu ilikuwa ni kumkaribisha na kumuaga,” alisema huku akimkabidhi vitabu na makabrasha kadhaa yaliyoandikwa Fifa.

Ndumbaro aliwahi kugombea nafasi ya Makamu wa Pili wa Rais wa TFF lakini akashindwa kwa kura chache na Ramadhani Nassib na sasa inaelezwa huenda akagombea nafasi hiyo ya Tenga ambayo tayari Jamal Malinzi na Athuman Nyamlani wamejitokeza.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic