August 13, 2013


Beki wa zamani wa Simba, Said Ndikumana ‘Koko’ amesema Simba imelamba dume kwa kumsajili Kaze Gilbert ‘Demunga’ raia wa Burundi.

Kokoo raia wa Burundi pia aliyeichezea Simba miaka mine iliyopita, amesema Demunga ni kati ya mabeki bora wachache wa kati katika ukanda wa Afrika Mashariki.

“Awali nilisikia Simba wanataka kumsajili, nikajua wanaweza wakachukulia kawaida tu.


“Lakini wamekuwa siriaz, kweli wamepata beki mzuri sana, ni mchezaji wa uhakika na ana uwezo mkubwa.

“Uchezaji wa Demunga ni kama Victor Costa, anapenda kutuliza mpira, anajiamini na ni mzuri kwa mipira ya vichwa. Kama watakaa naye vizuri, ninaamini watafurahia sana,” alisema Kokoo.

Kwa sasa Kokoo yuko mapumzikoni nyumbani kwao Bujumbura na anatarajia kurejea Oman alikokuwa anacheza soka la kulipwa.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic