August 13, 2013


Beki David Luiz amezua tafrani katika klabu yake baada ya kumueleza Jose Mourinho kwamba anataka kuondoka na kujiunga na Barcelona.

Luiz raia wa Brazil amezua mkanganyiko huo na kusisitiza anataka kuondoka ikiwa ni takribani wiki moja tu kabla ya kuanza kwa Ligi Kuu England.


Awali Barcelona ilitangaza kulipa pauni milioni 25, Chelsea ikaona ni kama kichekesho kwa kuwa ndiyo fedha iliyolipa kumpata kutoka Benfica ya Ureno.

Taarifa zinaeleza kuwa Kocha Tata Martino wa Barcelona atakuwa tayari kuongeza dau la pauni milioni 31, ili kumpata beki huyo.

Luiz sasa ni kati ya mabeki bora wa kati katika Ligi Kuu England na Barcelona inafanya kila juhudi kumpata ili kuziba pengo la Carles Puyol, nahodha wake wa zamani na beki imara zaidi wa kati.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic