Sakata
la usajili wa Luis Suarez limeingia katika sura mpya baada ya Mruguay huyo
kuzungumza na kusema hajui lolote kuhusiana na kubaki Livepool.
Suarez
amekanusha taarifa iliyochapishwa na gazeti la El Observador la Uruguay ambalo
lilimkariri kwamba amesema ameamua kusema anabaki.
Suarez
amesema hakuzungumza na mwandishi yoyote kuhusiana na suala hilo, hivyo haikuwa
sahihi.
Kauli
yake hiyo ina maanisha kuwa bado ana mpango wa kuiacha Liverpool pamoja na
kauli ya Kocha wake, Brendan Rodgers kumtaka aombe msamahe kwa wachezaji wote.
“Sikusema
lolote kuhusiana na kubaki, labda alizungumza na mtu yoyote, kikubwa kwa sasa
ni kwamba niko hapa na timu ya taifa na si zaidi,” alisema Suarez dakika chache
baada ya mechi kati ya timu yake ya taifa ya Uruguay dhidi ya Japan kumalizika,
yeye akiwa kati ya waliofunga.
Sakata
la mshambuliaji huyo mbaguzi wa rangi limekuwa likiendelea kuchukua kura mpya
na amekua akiwaeleza wazi kwamba anataka kuhamia Real Madrid ya Hispania.









0 COMMENTS:
Post a Comment