September 25, 2013





Kiungo mshambuliaji wa Azam FC, Joseph Kimwaga, ambaye aliifungia timu yake bao la ushindi kwenye mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara dhidi ya Yanga, Jumamosi, amesema majeraha yalimnyima nafasi ya kucheza Ulaya.


Kiungo huyo amesema alikuwa anatakiwa kwenda kucheza soka la kulipwa nchini Ureno.

Akizungumza na Championi Jumatano, kiungo huyo alisema alipata dili la kwenda kufanya majaribio nchini Ureno, lakini majeraha yakamnyima nafasi ya kucheza huko.
Kimwaga alisema klabu mbili zilijitokeza zikimhitaji kwa ajili ya majaribio, hivyo hajakata tama, badala yake ataendelea kufanya mazoezi kwa bidii ili kutimiza malengo yake ya kucheza soka la kulipwa.
 “Hivi karibuni nilipata ofa ya kuitwa kwenye klabu mbili za Ureno zikinihitaji kwenda kufanya majaribio ya kucheza soka la kulipwa, lakini ilishindikana kutokana na majeraha yaliyokuwa yananisumbua.
“Bado sijakata tamaa ya kucheza soka la kulipwa, ninaamini nitapata dili lingine la kwenda kucheza soka la kulipwa, najua kuwa nina uwezo mkubwa wa kucheza soka, pia nimefurahi sana kumfunga bingwa wa msimu uliopita wa ligi kuu,” alisema Kimwaga, 20.

Katika mchezo huo uliomalizika kwa Yanga kulala kwa mabao 3-2, Kimwaga aliifungia timu yake bao la tatu dakika za mwisho kabisa za mchezo huo.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic