September 25, 2013





Javier Harnandes amefunga bao pekee katika mechi ya Kombe la Capital One raundi ya tatu kati ya Liverpool dhidi ya Man United.


Man United waliokuwa nyumbani OT walipata ushindi huo wa bao 1-0 baada ya kona iliyochongwa na Wayne Rooney kumpita Steven Gerrard na kutua mguuni mwa Chicharito.


Ukichana na bao hilo, mchezo wa timu zote ulilingana na mashambulizi yalikuwa ya zamu.


Luis Suarez aliyekuwa amerejea Liverpool kwa mara ya kwanza baada ya kumaliza adhabu ya kufungiwa ya FA, alionyesha yuko fiti lakini hakuweza kuisaidia Liverpool kusawazisha.

Mara moja mpira wa adhabu wa Mruguay huyo ulipalaza mtambaa wa panya na wakati mwingine kipa David De Gea akaokoa mpira wa kichwa wa karibu kabisa wa Victor Moses.



Kwa upande wa Arsenal, wao walitotoka sare ya bao 1-1 dhidi wa Wes Brom Albioni katika kali ya kusisimua.

Vijana hao wa Wenger walikuwa ugenini na bao lao lilifungwa na Thomas Eisfeld na wenyeji wakasawazisha kupitia Thomas Seido.

Kutokana na matokeo hayo, waliongezewa muda wa dakika 30 ili kupata mshindi, hadi tunakwenda mitamboni ilikuwa bado 1-1.

MATOKEO MENGINE CAPITAL ONE
Birmingham 3 Swansea 1
Newcastle 2 Leeds 0
Tranmere 0 Stoke 1

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic