September 25, 2013




Kiungo nyota wa Yanga, Athumani Idd ‘Chuji’ amelazimika kuondoka katika kikosi hicho kwa muda.

Uongozi wa Yanga umempa Chuji ruhusa ya siku mbili kwenda kumzika shangazi yake mjini Mpwapwa mkoani Dodoma.
“Kweli Chuji amefiwa na shangazi yake na anakwenda kushiriki mazishi.


“Amepewa ruhusa na baada ya hapo atarejea na kuungana na wenzake,” alisema Meneja wa Yanga, Hafidh Saleh.

Chuji ni kati ya viungo wakongwe wa Yanga na amekuwa tegemeo katika kuituliza na uchezeshaji wa timu.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic