September 25, 2013





Hatimaye uongozi wa Yanga umejinusuru na adhabu kutoka kwa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), kufuatia kuwalipa waliokuwa wachezaji wao, Stephano Mwasyika na Shadrack Nsajigwa ‘Fusso.’

Taarifa ambazo zimelifikia Championi Jumatano kutoka kwa mmoja wa viongozi wa juu wa klabu hiyo, imesema tayari uongozi wao umeshamalizana na nyota hao kwa kuwalipa fedha zote walizokuwa wakiidai klabu hiyo, ambazo ni jumla ya Sh million 15.5 za usajili.


Bosi huyo (jina tunalo), amesema tayari wachezaji wote wameshachukua hundi zao za malipo ya madeni hayo. Fusso ambaye alikuwa nahodha wa timu hiyo, alikuwa akiidai Yanga kiasi cha Sh milioni 9 wakati Mwasyika, anayekitumikia kikosi cha Ruvu Shooting kwa sasa, alikuwa akidai Sh milioni 6.5.

“Hatukuona haja ya kulumbana nao sana, tayari tumeshawalipa fedha zote wiki hii, nafikiri kila mmoja mpaka sasa atakuwa tayari ameshachukua hundi yake,” alisema bosi huyo.

Kufuatia kauli hiyo ya bosi huyo, Championi Jumatano lilimtafuta Fusso katika kujua ukweli, ambapo alisema: “Ni kweli wameshanilipa fedha zangu, siyo kwa nusunusu, binafsi wamenilipa zote, hakuna tatizo sasa.”

Nyota hao ambao waliachwa na Yanga mwishoni mwa msimu uliopita, walipeleka malalamiko yao TFF wakidai fedha hizo, baadaye Kamati ya Sheria, Maadili na Hadhi za Wachezaji iliyokaa Septemba 12, mwaka huu, ikaamuru klabu hiyo ilipe madeni hayo ndani ya siku 14.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic