September 25, 2013



 
SIWA (KULIA) AKIWA NA MENEJA WA YANGA, HAFIDHI SALEH

Kocha wa Makipa wa Yanga, Razack Siwa, tayari amehakikishiwa kupewa nyumba ya kifahari na usafiri wa ndani iwapo atajiunga na Mjees FC ya nchini Oman.


Akizungumza na Championi Jumatano, Siwa ambaye ni raia wa Kenya, alisema amekwishaahidiwa kupata nyumba ya kifahari ambayo atakuwa akiishi yeye na familia yake kwa kipindi chote atakachokuwepo katika klabu hiyo.

Alisema pia tayari ameshahakikishiwa usafiri wa nguvu atakaokuwa akiutumia ndani ya nchi hiyo kwa ajili ya kurahisisha masuala madogomadogo kama mitoko na mengineyo.

“Wameahidi kunipa nyumba ya kifahari na usafiri wa nguvu utakaokuwa unanizungusha mimi na familia yangu kwenda mazoezini au katika mizunguko binafsi na nimekubaliana nao kuhusu hilo, ninachosubiri ni malipo.

“Hao jamaa wameniambia wanakaa kikao kujadili mshahara ambao ninautaka, wamefikia pazuri na siyo muda sana nitaondoka hapa Yanga,” alisema Siwa.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic