September 27, 2013





Baada ya kurudi nchini akitokea India kufanyiwa upasuaji wa goti, kiungo wa Simba, Kiggi Makasi, atalazimika kuwa nje ya uwanja kwa muda wa miezi mitatu ili kupona majeraha yake.


Kiggi alikwenda India, Septemba 9, mwaka huu kufanyiwa upasuaji wa goti aliloumia kwenye mechi ya kirafiki dhidi ya CDA ya Dodoma mapema mwaka huu.

Daktari wa Simba, Yassin Gembe alisema: “Anaendelea vizuri ambapo kwa mujibu wa madaktari wa India atatakiwa kupumzika kwa muda wa miezi mitatu kisha ndiyo ataanza mazoezi mepesi.”

Aidha, taarifa kutoka ndani ya klabu hiyo zinaeleza kuwa, gharama zote alizotumia mchezaji huyo akiwa India kwa matibabu na mambo mengine ni shilingi milioni 15.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic