September 27, 2013






Beki wa zamani wa Yanga, Shadrack Nsajigwa ambaye alikuwa kocha mkuu wa Lipuli FC ya Iringa, ameamua kuachana rasmi na timu hiyo inayoshiriki Ligi Daraja la Kwanza Tanzania Bara ikiwa ni siku chache tangu aanze kibarua hicho.
  
Nsajigwa amefikia uamuzi huo wa haraka kutokana na mazingira magumu ya ufundishaji aliyokuwa akikutana nayo huku uongozi wake ukionekana kutojali.


Inaelezwa kuwa Nsajigwa hakutimiziwa mahitaji ya mechi ambayo alihitaji ili kurahisisha kazi yake ya ufundishaji lakini akawa hatekelezewi.

“Wiki iliyopita alirejea Dar akitokea Iringa baada ya kupata matatizo ya kifamilia, kipindi hicho anaaga alikuwa tayari ameshamwambia mmiliki wa timu hiyo kuwa amechoshwa na maisha ya hapa, hivyo aliomba kuondoka mwenyewe.
“Alipofika Dar kuna jamaa yake akamtaarifu kuwa ni bora asirejee Iringa kwa kuwa baadhi ya viongozi waliweka mikakati ya kumchafua katika mechi dhidi ya Kimondo itakayochezwa kesho Jumamosi,” alisema mtoa habari wetu.
Alipoulizwa Nsajigwa kuhusiana na taarifa hizo alisema: “Ni kweli nimeachana na timu hiyo, hivi sasa ninavyozungumza na wewe nipo Dar ninafanya mambo  yangu binafsi.”

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic