Na Saleh Ally
Uhamisho wa wachezaji wawili,
Neymar kutoka Santos ya Brazil kwenda Barcelona na Gareth Bale kutua Madrid
akitokea Tottenham, ndiyo umekuwa gumzo zaidi duniani.
Wachezaji hao wawili walikuwa
nyota na tegemeo katika timu zao na walipojiunga na Real Madrid na Barcelona
walikutana na magwiji wa timu hizo, Cristiano Ronaldo na Lionel Messi.
Wengi walikuwa wanajiuliza
namna ambavyo wangeweza kucheza pamoja au wangeweza vipi kutamba zaidi ya
wakali hao ambao wamekuwa wachezaji nyota zaidi si katika La Liga pekee, bali
duniani kote.
Bale amekuwa gumzo zaidi
kutokana na kuweka rekodi ya uhamisho wa pauni milioni 86 (Sh bilioni 224),
ndiye mchezaji ghali zaidi duniani. Lakini pamoja na kwamba Neymar alilipiwa
pauni milioni 50 ambayo ni zaidi ya Sh bilioni 130 (kutua Barca ambazo si haba,
wengi walisubiri ligi itakapoanza.
Watalaamu kadhaa wakiwemo makocha
wa zamani walisema ingekuwa vigumu kwa Neymar kucheza na Messi na kung’ara,
lakini kuna ambao walisisitiza angeweza na kwa pamoja watafanya vizuri.
Kwa upande wa Ronaldo na Bale,
ilionekana wangeweza kufanya kazi pamoja lakini swali lilikuwa hivi: Kati ya
wawili hao nani atang’ara zaidi ya mwenzake?
Suala la nani atakuwa zaidi
hata kwa upande wa Messi na Neymar lilichukua nafasi, wengi walichambua na
kusisitiza Neymar atachukua nafasi kubwa na kuiongoza Barcelona huku ‘mwenyeji’
wake akiporomoka.
Tayari mechi sita kwa kila timu
za La Liga zimeishachezwa, uchambuzi na mawazo yaliyotolewa yanaonekana
‘kukosea njia’ kwa kuwa wenyeji Messi na Ronaldo wanaonyesha wao ndiyo wenye
‘nchi’.
Wanaendelea kufanya vizuri
zaidi huku Bale na Neymar wakijikongoja kwa dalili ambayo si mbaya, kwamba wana
uwezo wa kufanya vizuri, lakini bado wanahitaji muda kwa kuwa La Liga ina wenyewe.
Mechi sita pekee zinaweza kuwa
chache lakini takwimu ndizo zinazoonyesha yupi ni mkali kati ya wenyeji na
wageni.
Inawezekana mechi sita zikawa
ni chache, huenda wageni wakageuka baadaye, lakini hakuna ubishi, biashara ni
asubuhi na kama wameanza hivyo, basi watafika mbali zaidi.
Messi anaongoza katika ufungaji
mabao akiwa na saba, Ronaldo anafuatia akiwa na sita na Neymar na Bale kila
mmoja wao ana bao moja tu.
Ingawa Bale anaweza kusema
hajapata nafasi ya kucheza mechi nyingi kutokana na kuwa majeruhi lakini ukweli
unabaki palepale, ana bao moja.
Kitu kingine utaona ni idadi ya
mashuti waliyopiga langoni, wanapishana kwa idadi kubwa. Mwenyeji Messi amepiga
langoni mashuti 32 wakati mgeni wake Neymar amepiga 15 tu. Ronaldo ana mashuti
48 na Bale mawili tu.
Hali halisi inaonyesha wageni
hao yaani Neymar na Bale wanahitaji nguvu na juhudi kuhakikisha wanakuwa
washindani sahihi. Angalia takwimu za wanne hao baada ya La Liga kufikisha
mechi sita, Barcelona ikiwa kileleni, ikifuatiwa na Atletico Madrid na Real
Madrid.
Ukizungumzia kasi ya mabao timu
zote mbili zinaonyesha kuwa kwenye kasi lakini Barcelona ndiyo ambayo imekuwa
juu zaidi, kwani mpaka sasa imefunga mabao 22 na kufungwa matano wakati Madrid
wamefunga 14 na kufungwa sita. Hiyo inaonyesha kazi imeanza kwa mwendo mkali
kama ambavyo imekuwa ikifanyika misimu ya hivi karibuni.
- MESSI
|
MECHI
|
MABAO
|
PASI
|
MASHUTI
|
|
5
|
7
|
3
|
32
|
- NEYMAR
|
MECHI
|
MABAO
|
PASI
|
MASHUTI
|
|
6
|
1
|
4
|
15
|
- RONALDO
|
MECHI
|
MABAO
|
PASI
|
MASHUTI
|
||||
|
6
|
6
|
1
|
48
|
||||
- BALE
|
MECHI
|
MABAO
|
PASI
|
MASHUTI
|
||||
|
1
|
1
|
0
|
2
|
||||









0 COMMENTS:
Post a Comment