September 28, 2013





Kocha Jose Mourinho wa Chelsea amemtaka Andre Villas-Boas wa Tottenham kumheshimu na kuachana na maneno mengi.


Mourinho raia wa Ureno kama ilivyo kwa AVB amesema amemfundisha mambo mengi kocha huyo anayopaswa kujivunia sasa.


Amesema anashangazwa na maneno mengi anayotoa AVB aliyekwua msaidizi wake akiwa Chelsea na amesahau mengi aliyomfundisha yanayomfanya aonekane moja ya makocha wazuri.

Amesema alikuwa akimfudisha kila kilicho sahihi wakati wakifanya kazi wote na anatakiwa kuonyesha shukurani badala ya maneno mengi yanayoonyesha kumvunjia heshima.
Mourinho ndiye alimchukua AVB akaajiliwa Chelsea katika kitengo cha kusaka vipaji kuanzia 2004 hadi 2009 yeye alipohamia Inter Milan.

Hivi karibuni AVB amekuwa akisukuma maneno yanayoonyesha wazi kumshambulia Mourinho.

Lakini Mourinho amesisitiza: “Sitaki kusikiliza anachosema ni nini, lakini hali halisi inajionyesha. Zaidi ninachojua asilimia 90 ya wanaonizungumzia huwa hawanifahamu wala hawajui nilivyo.”

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic