Mshambuliaji wa Yanga, Mrisho Ngassa ametaka apumzishwe na maneno ili afanye kazi yake.
Ngassa amesema anataka kuelekeza nguvu yake katika kikosi cha Yanga, hivyo hahitaji malumbano.
“Ningependa nicheze soka, najua ndiyo ninaanza kuichezea timu yangu hivyo sipendi kuingia kwenye malumbano.
“Nasikia maneno mengi, lakini si jambo zuri kwangu. Vizuri waniache nifanye kazi,” alisema.
Jana, Ngassa alikwenda TFF na kukabidhi fedha Sh milioni 45 zilizokuwa sehemu ya adhabu yake.
Sasa amemaliza adhabu la leo ataanza kuichezea Yanga rasmi katika mechi dhidi ya Ruvu Shooting.







0 COMMENTS:
Post a Comment