September 24, 2013

HOLLAND AKIWA NA MOURINHO KATIKA BENCHI LA CHELSEA..
Msaidizi wa Kocha José Mourinho aitwaye Steve Holland amesema mshambuliaji wa Real Madrid, Cristiano Ronaldo alibadilika na kuwa wa kiwango cha juu zaidi alipokuwa akifanya kazi na kocha huyo.


Holland ambaye sasa ni msaidizi wa Mourinho katika kikosi cha Chelsea amesema kocha huyo Mreno amefanya kazi kubwa kumbadili Ronaldo.

“Utaona namna alivyobadilika katika kipindi cha miaka mitatu iliyopita na kuwa tishio, Mourinho anajua namna ya kumbadilisha mchezaji.

“Amemfundisha Ronaldo mambo mengi ya msingi ambayo hakika yalimbadili na kumfanya awe tishio duniani, anapaswa kumshukuru Mourinho katika hilo,” alisema Holland.


Mourinho alifanya kazi na Ronaldo wakati wakiwa Real Madrid na sasa ametua Chelsea ambayo aliwahi kuifundisha kabla.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic