September 16, 2013



 
MULUGO AKIKABIDHI KITITA HICHO
Timu ya Mbeya City ya jijini hapa, imekabidhiwa fedha taslimu Sh milioni moja baada ya kufanikiwa kuibana Yanga kwa kuilazimisha sare ya bao 1-1.


Aliyetoa mkwanja huo ni Mbunge wa Jimbo la Songwa mkoani hapa, Philipo Mulugo ambaye pia ni Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi. Mulugo ni mdau mkubwa wa soka mkoani hapa.

Mbeya, juzi ilitoka sare ya kufungana bao 1-1 na Yanga kwenye mchezo uliopigwa katika Uwanja wa Sokoine jijini hapa.

Mulugo alisema  aliahidi kuipa timu hiyo Sh milioni mbili kama ingeibuka na ushindi lakini kwa kuwa ilitoka sare, ametoa Sh milioni moja.

“Si matokeo mabaya, ni matokeo safi, lakini niliahidi kama wangeshinda basi ningewapa mbili ila kwa kuwa wamedroo basi nimewapa moja kama pongezi kwao kwa mchezo mzuri waliouonyesha,” alisema Mulugo.

Fedha hizo alikabidhiwa kocha mkuu wa timu hiyo, Juma Mwambusi.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic