September 29, 2013


Pamoja na kuwa na wachezaji wake wote nyota, Real Madrid imeonja kipigo cha kwanza cha La Liga.
Madrid imefungwa 1-0 na wapinzani wake wakubwa Atletico Madrid tena ikiwa kwenye uwanja wa nyumbani wa Santiago Bernabeu.

Bao hilo pekee lililoacha majonzik na kipigo cha kwanza kwa kikosi cha Carlo Ancelotti lilifungwa na Diego Costa katika dakika ya 11.


Kutokana na ushindi huo, Atletico Madrid iliendelea kubaki nafasi ya pili ikiwa na pointi 21 sawa na vinara Barcelona wakati Madrid inabaki nafasi ya tatu.


Katika kipindi cha pili Madrid walishambulia mfululizo lakini mwisho wakaambulia kipigo hicho kutoka kwa watani wao hao wa jadi wanaonolewa na Diego Simione, kiungo wa zamani wa nyota Argentina.

Real Madrid Diego Lopez, Arbeloa, Ramos, Pepe, Coentrao, Illaramendi, (Modric 45) Di Maria (Bale 45), Isco, Ronaldo, Benzema (Morata 73).
Subs Casillas, Carvajal, Casemiro, Varane
Atletico Madrid Courtois, Juanfran, Miranda, Godin, Filipe Luis, Koke, Tiago, Gabi, Arda Turan, Diego Costa, Villa
Subs Aranzubia, Alderweireld, Guilavogui, Rodriguez, Oliver, Garcia, Baptistao



0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic