September 27, 2013





Beki Mtanzania, Shomari Kapombe wa AS Cannes, ameongezewa muda wa mapumziko hadi mwezi ujao.

Kitengo cha afya cha klabu hiyo, kimetangaza kuwa Kapombe ambaye alifanyiwa upasuaji wa kidole, analazimika kusubiri zaidi kabla ya kuanza mazoezi.


“Atakuwa nje zaidi hadi Oktoba, tutaangalia afya yake na baada ya hapo tutaeleza ataanza lini mazoezi,” alisema Pierre ambaye ni mmoja wa wahusika wa kitengo hicho, alipozungumza na Championi Ijumaa, jana.

“Baada ya kufanyiwa upasuaji, tuliona hakuwa amepona vizuri hata baada ya zile siku tulizoamini zinatosha. Hivyo tumempa siku zaidi lakini kama nilivyosema matarajio ni hadi Oktoba.”

Awali AS Cannes inayoshiriki Ligi Daraja la Nne nchini Ufaransa, ilitangaza Kapombe atakuwa nje ya uwanja kwa siku 15 kutokana na kufanyiwa upasuaji wa kidole ambacho kilikuwa kinamsumbua na ikafikia hadi akashindwa kuvaa viatu.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic