October 9, 2013





 Azam imefanikiwa kujiongezea pointi tatu muhimu baada ya kuichapa Mgambo Shooting kwa mabao 2-0.

Katika mechi hiyo ya Ligi Kuu ya Vodacom iliyochezwa kwenye Uwanja wa Chamazi jijini Dar, leo. Timu hizo zilikwenda mapumziko zikiwa sare ya 0-0.


Kipindi cha pili mambo yalibadilika na kupitia kwa Farid Malik aliyeingia kuchukua nafasi ya Mganda, Bryan Umonyi.

Dakika ya 85, Kipre Herman Ttchetche akaifungia Azam Fc bao la pili kwa mkwaju wa penalti.

Kwa ushindi huo Azam FC imechuka hadi nafasi ya pili ikiwa na pointi 14 nyuma ya vinara Simba wenye 15 na kufuatiwa na Yanga na JKT zenye 12 kila moja.

Hata hivyo, Azam FC ina mchezo zaidi baada ya kucheza nane wakati timu nyingine zina mechi saba.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic