October 31, 2013


Vurugu kubwa zimeibuka wakati wa mechi ya Bara kati ya wenyeji Simba na Kagera Sugar kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar.

Vurugu hizo zimetokea mara tu baada ya mwamuzi kupuliza kipyenga kuashiria mpira kwisha mara tu baada ya Kagera Sugar kupata bao la kusawazisha lililofungwa na beki Salum Kanoni kwa mkwaju wa penalty.


Mashabiki wa Simba walianzisha vurugu wakipinga mwamuzi kutoa penalty hiyo ikiwa ni baada ya Simba kufanikiwa kupata bao katika dakika ya 44 mfungaji akiwa Amissi Tambwe.

Bao hilo lilidumu hadi mapumziko na kipindi chote hakukuwa na bao hadi wakati wa dakika za nyongeza, Paul Ngwai alipoangushwa kwenye eneo la hatari.

Matokeo hayo ya bao 1-1 yalionyesha kuwakera mashabiki walioanzisha vurugu hizo, wakivunja viti hali iliyosababisha askari uwanjani hapo watupe mabomu ya machozi na amani ikapotea.

Baadhi ya watu walizimia na wengine kuumia na watu wa Msalaba Mwekundu wakaanza kutoa huduma ili kuokoa maisha yao.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic