KABANGE |
Kocha Mkuu wa Kagera Sugar, Mlage
Kabange amemuambia bosi wake wa zamani, Abdalla Kibadeni asitegemee mchekea katika mechi ya leo.
Kagera Sugar watakuwa wageni wa Simba
kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar kuendelea kusaka pointi tatu muhimu za Ligi
Kuu Bara.
Kabla ambaye alikuwa msaidizi wa
Kibadeni wakati akiwa Kagera Sugar, amesema wamejiandaa vizuri na Simba
wategemee mechi ngumu na ikiwezekana kupoteza.
“Najua Simba watakuwa wazuri kwa kuwa
wana kocha mzuri, lakini lazima wapate upinzani mkali na kweli sisi tunataka
kushinda.
“Kibadeni ni kocha mzuri na alipokuwa
Kagera ameniachia urithi wa baadhi ya mambo muhimu. Lakini leo kila mtu atakuwa
kazini na kutaka kushinda,” alisema Kabange ambaye pia ni mchezaji nyota wa
zamani.
0 COMMENTS:
Post a Comment